
Magonjwa
Sumu ya kunywa maji mengi kupita kiasi
Kunywa maji mengi kupitiliza
Haishauriwi kiafya kunywa maji mengi zaidi ya mahitaji ya mwili wako kwa kuwa kiwango kinachozidi huweza geuka kuwa sumu. Kwa bahati mbaya dalili za sumu ya maji kutokana na kunywa maji mengi huwa ngumu kutambuliwa kirahisi na wataalamu wa afya kwa kuwa dalili zake hufanana na magonjwa ya akili, endapo tatizo lisipofahamika mapema na kupata tiba huleta madhara makubwa pamoja na kifo.
Tatizo la sumu ya maji linalotokea kutokana kuwa na maji mengi mwilini kuliko kiwango cha chumvi hutokea kwa nadra na huweza pelekea kifo.
Dalili za mtu aliyekunywa maji mengi kupitiliza
Tetekuwanga
Tetekuwanga ni ugonjwa unaosababshwa na kirusi Varicella zoster AU kirusi tetekuwanga. Ugonjwa huu husababisha harara ndogo na malenge kwenye ngozi yanayoambatana na muwasho.
Dalili za tetekuwanga
Tetekuwanga huonekana siku 10 hadi 21 baada ya kupata maambukizi. Dalili kuu ya ugonjwa huu huwa ni malengelenge madogo yanayowasha na hudumu kwa muda wa siku 5 hadi 10. Dalili zingine zinazoonekana siku 1 hadi 2 kabla ya kuona vipele ni;
Homa
Kukosa hamu ya kula
Maumivu ya kichwa
Homa baada ya chanjo
Kwanini homa hutokea baada ya chanjo?
Chanjo hutayarisha mfumo wa kinga ya mwili kuulinda mwili dhidi ya virusi au bakteria wanaoweza kuleta ugonjwa. Homa hii hutokea kwa sababu chanjo huwa na viunda vya vijidudu hivyo ambavyo vinajulikana kuamsha mwitikio wa kinga ya mwili. Hata hivyo, chanjo huwa hazisababishi mwitikio wa unaoweza kumfanya mtu kuugua ugonjwa kama wanavyosababisha vimelea asili. Kwa baadhi ya watu, mwitikio wa kinga ya mwili huwa na nguvu ya kutosha kusababisha dalili zinazoweza kuonekana kama vile homa kali.
Nini unapaswa kufanya unapopata homa?
Mara nyingi si lazima kutumia dawa za kushusha homa kama vile paracetamol unapopatwa na homa baada ya kuchoma chanjo. Inashauriwa kunywa maji ya kutosha tu wakati huu. Kama unafikiria homa ni kali au inakupelekea kukulaza, wasiliana na daktari wako kwa ushauri na tiba.
Rejea za mada hii:
Ahn SH, Zhiang J, Kim H, Chang S, Shin J, Kim M, Lee Y, Lee JH, Park…