top of page

USHAURI WA MATUMIZI YA DAWA KIPINDI CHA  UJAUZITO NA KUNYONYESHA

Lamivudine na ujauzito

Lamivudine na ujauzito

Taarifa za wanyama na binadamu zinapendekeza dawa hii kuwa kwenye kundi la sawa zenye hatari kidogo kusababisha madhaifu ya kiuumbaji kwa kijusi tumboni mwa mama.

Amoxicillin na ujauzito

Amoxicillin na ujauzito

Kuna ushahidi kuwa matumizi ya dawa hii kwenye kipindi cha kwanza cha ujauzito husababisha vichanga kuzaliwa na tatizo la mdomo sungura licha ya hatari hii kuwa ndogo.

Erythromycin na ujauzito

Erythromycin na ujauzito

Ripoti za tafiti nyingi ikiwa pamoja na tafiti kwa wanyama hazijapata ushahidi wa kutosha kuwa ni sumu kwenye ukuaji wa kichanga endapo mjamzito atatumia erythromycin licha ya ripoti moja kusema kuwa ina inasababisha ulemavu wa moyo kwa vichanga.

Ticarcillin-clavulanic acid  kwa ujauzito

Ticarcillin-clavulanic acid kwa ujauzito

Tafiti nyingi zimeonyesha kutokuwepo kwa madhara kwa kijusi na mtoto anayezaliwa na mama aliyetumia dawa hii.

Amoxiclavu na ujauzito

Amoxiclavu na ujauzito

Tafiti nyingi zimeonyesha kutokuwepo kwa madhara kwa kijusi na mtoto anayezaliwa. Hata hivyo tafiti moja imeripoti kuwa kuna mahusiano kati ya matumizi ya dawa hii na kutokea kwa ugonjwa wa kuoza kwa utumbo wa mtoto kwa vichanga wanaozaliwa.

Cephalexin kwenye ujauzito

Cephalexin kwenye ujauzito

Cephalexin antibayotiki kundi la cephalosporin, dawa hii hutumiwa kwa kunywa. Tafiti za panya zimeonyesha kuwa cephalexin haina madhara kwa kijusi tumboni kwenye dozi ya miligramu 500 kwa kilo, dozi inayoweza pelekea kuingilia uumbaji wa kijusi cha panya akiwa tumboni.

Ingawa dawa hii imeonekana kutosababisha madhara ya kimaumbile kwa mtoto, tafiti moja imeleta mkang’anyiko kwa kuonyesha kuwa dawa cephalexin inahusiana na madhaifu ya kiuumbaji kwa kijusi ambayo ni madhaifu ya moyo, tatizo la mgongo wazi, kuzaliwa na vidole vingi, kupungua kwa mikono au miguu, na haipospadiasisi.

Madhara haya kwenye tafiti yamelezewa kuhusiana na matatizo waliyokuwa nayo wazazi, matumizi ya dawa zingine au mambo mengine.

Tafiti nyingine pia imeonyesha kuhusiana na madhaifu ya moyo na mdomo sungura kwa watoto wa mama waliotumia dawa hii kwenye ujauzito.

Kiasi kidogo huingia kwenye maziwa ya mama na humpata mtoto na kuleta madhara ya kubadilisha bakteria rafiki kwenye mfumo wa tumbo la mtoto, kutoa majibu ya kuotesha bakteria yasiyo sahihi endapo mtoto ana homa na madhara ya moja kwa moja kwa mtoto. Tafiti moja inaonyesha kuwa mama alipotumia dawa hii pamoja na probenecid ilihusiaa na madhara kwa mtoto. Hata hivyo wataaluma wameweka dawa hii kuwa salama kutumika kwa mama aonyonyesha.

Ingawa baadhi ya tafiti zimeonyesha kuhusiana na madhaifu ya kiuumbaji kwa mtoto, kwa ujumla imeonekana kuwa ni salama kutumika wakati wa ujauzito.

Cefuroxime na ujauzito

Cefuroxime na ujauzito

Tafiti kwenye panya zimeonyesha dawa haina madhara kwenye uzazi kwenye dozi iliyotumika ambayo ni sawa na mara 9 ya dozi inayotakiwa kutumika kwa binadamu, panya, na nyani.

Ceftriaxone na ujauzito

Ceftriaxone na ujauzito

Ceftriaxone ni dawa ya antibiotiki ya kuchoma iliyo katika kundi la cephalosporin. Tafiti za panya zimeonyesha dawa haina madhara kwenye uzazi kwenye dozi iliyotumika ambayo ni sawa na mara 20 ya dozi inayotakiwa kutumika kwa binadamu, panya, na nyani.

Emtricitabine na ujauzito

Emtricitabine na ujauzito

Taarifa za wanyama zinaonyesha kuwepo kwa hatari kiasi, hata hivyo taarifa chache zilizopo kuhusu matumizi yake zinafanya kutokuwa na majibu ya uhakika kuhusu madhara kwa kijusi na kichanga tumboni.

Thiamine na ujauzito

Thiamine na ujauzito

Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa thiamine ni salama wakati wa ujauzito endapo itatumika katika dozi inayoruhusiwa kutumika katika ujauzito.

Telbivudine na ujauzito

Telbivudine na ujauzito

Kuna taarifa chache kuhusiana na matumizi ya dawa hii kwa binadamu wajawazito. Ingawa taarifa za wanyama wajawazito zinatia moyo, taarifa za binadamu wajawazito zinatakiwa kupatikana ili kutoa hitimisho kuhusu usalama wake kwenye ujauzito wa binadamu.

Tenofovir na ujauzito

Tenofovir na ujauzito

Ingawa taarifa za wanyama zinaonyesha hatari kwenye ujauzito kwa kupunguza ukuaji wa kichanga, taarifa hazijitoshelezi kutoa ushauri kuhusu dawa kusababisha madhaifu ya kiuumbaji.

bottom of page