top of page

Majibu ya maswali mbalimbali

Kipimo cha mimba kwenye mkojo huanza kuonesha uwepo wa mimba baada ya muda gani?

Kipimo cha mimba kwa kutumia mkojo hupima uwepo wa homoni hCG ambayo huzalishwa kwa wingi wiki kadhaa baada ya kukosa hedhi. Huchukua takribani siku 14 tangu kukosa hedhi kipimo kuweza kuonesha ujauzito.

Kuna aina ngapi za seli mundu?

Seli mundu ni ugonjwa wa kurithi unaoathiri seli nyekundu za damu. Zipo aina kuu nne za seli mundu kulingana na vinasaba alivyorithi mtu.

Kikohozi cha UKIMWI

Je, kikohozi cha UKIMWI kikoje?

Ingawa kikohozi kikavu ni dalili mojawapo ya maambukizi ya HIV, hutakiwi kuhofu endapo una dalili hii na umejianika kwenye kihatarishi kwa kuwa kinaweza kusababishwa na sababu zingine.

Je unaweza kushiriki ngono wakati unatumia PEP?

Unashauriwa kutoshiriki ngono wakati unatumia PEP ili kujikinga na maambukizi mapya pamoja na kumkinga mwenza wako dhidi ya maambukizi, ikishindikana, tumia kondomu.

Maambukizi ya VVU

Je, kwenye dirisha la matazamio unaweza kuambukiza VVU?

Ndio, unaweza kumwambukiza mtu mwingine VVU kabla ya kutambulika kwa kipimo endapo kuna kihatarishi kikuu cha maambukizi.

Dalili kuu na dalili ambata

Je, wamsaidiaje daktari kutambua ugonjwa kwa dalili?

Ili kutengeneza mawasiliano mazuri ya kutambua, kuchunguza na kukupa matibabu yanayoendana na shida yako, unapaswa kuelezea vema dalili kuu na dalili ambata.

Kutambua PID

Je, unatumbua vipi kama una PID?

Hakuna kipimo cha moja kwa moja cha kutambua PID, utambuzi wa sasa hutegemea dalili ulizonazo sambamba na uchunguzi wa mwili pamoja na vipimo vingine.

Kuna uwezekano wa kupona PID

Je, PID inatibika?

PID hutibika na kuisha kabisa endapo itagunduliwa mapema na kutibiwa kwa dawa sahihi. Hata hivyo matibabu hayaondoi madhara na uharibifu wowote uliokwisha tokea kwenye mfumo wa uzazi kutokana na ugonjwa.

Madhara ya kunguni

Kunguni husababisha madhara gani mwilini?

Kunguni ni mdudu anayejipatia chakula kwa kufyonza damu ya binadamu. Japokuwa hana madhara makubwa mwili, huweza kusababisha mzio kwenye ngozi kwa baadhi ya watu.

Ukimwi kwa kung'atwa na mwathirika

Unaweza kuambukizwa VVU kwa kung'atwa na mwathirika?

Maambukizi ya VVU yanaweza kutokea endapo kidonda cha kung'atwa kimekutana na majimaji, damu, shahawa, ute wa uke, uume au njia ya haja kubwa kutoka kwa mwathirika.

VVU kwa kushikana mikono

Maambukizi ya VVU kwa kushikana mikono

Vipo visa vichache vilivyoripotiwa kusababishwa na njia hii kiasi cha kuonekana kuwa na hatari kidogo ya maambukizi. Uambukizaji kwa njia hii hutegemea mambo mbalimbali baina ya mwathirika na anayeambukizwa

Fluconazole

Fluconazole katika tiba

Ni moja ya dawa inayotumika kutibu magonjwa mbali mbali yanasobabishwa na fangasi.

bottom of page