Kuhisi Mapigo ya moyo kwenda ndivyo sivyo baada ya kula (kwenda kasi/ haraka haraka au kwenda taratibu sana) husababishwa na moyo kuruka au kuongeza pigo moja. Mtu anaweza kuhisi mapigo ya moyo yanaenda ndivyo sivyo kwenye maeneo ya kifuani, shingoni au kooni kwa kupata hisia za kugongagonga au kupwita pwita. Vitu vingi huweza kusababisha mapigo ya moyo kwenda kasi kama dawa aina fulani, mazoezi makali/magumu, na chakula aina Fulani. Mapigo ya moyo kwenda kasi pia husababisha mapigo ya mishipa ya damu kupiga kwa nguvu.
Kupata hisia za Mapigo ya moyo kwenda kasi mara nyingi haimaanishi kuwa kuna tatizo kwenye mwili au kuna ugonjwa mkubwa unaoendelea ndani ya mwili. Hutakiwi kuwa na hofu kwani au kuhangaika kutafuta tiba, cha msingi fanya uwezavyo kukinga kisababishi mfano acha kunywa vinywaji vya kuongeza nguvu, vyakula vyenye karafuu, kahawa na baadhi ya madawa, jaribu kufanya mazoezi na kuvuta hewa/kupumua kwa kina zaidi.
Endapo mapigo ya moyo yamekuwa ndivyo sivyo na yanaambatana na dalili za kuishiwa pumzi, kizunguzungu, maumivu ya kifua au kuzimia, unatakiwa kuonana na daktari kwa uchunguzi zaidi.
Visababishi
Vitu au mambo yanayoweza sababisha mapigo ya moyo kwenda kasi vinaweza kuwa vya aina kadhaa , vingine vina uhusiano na matatizo ya moyo au kutohusiana na moyo au sababu kutojulikana kabisa. Sababu zisizo husiana na moyo ni;
Hisia kali kama huzuniko au huzuni
Kufanya kazi za kuutumikisha mwili kwa upesi sana
Vyakula vyenye karafuu, nikotini, pombe na madawa ya kulevya kama kokaine
Magonjwa kama ugonjwa wa upungufu wa homoni ya thyroid, sukari kuwa chini kwenye damu, upungufu wa damu, shinikizo la chini la damu, na kuishiwa maji mwilini.
Madawa kama madawa ya kuongeza au kupunguza hamu ya kula, pumu, kuponya mafua,dawa za kutibu moyo na dawa za kutibu upungufu wa homoni ya thyroid
Madawa ya mizizi na dawa za kuongeza virutubisho mwilini
Kuwa na kiwango cha madini mwilini kisicho cha kawaida, kinaweza kuwa cha juu au cha chini
Baadhi ya visababishi vya mapigo ya moyo kwenda ndivyo sivyo ni magonjwa ya moyo, mfano mshiko wa moyo, magonjwa ya mishipa ya moyo ya coronary, moyo kuferi, magonjwa ya milango ya moyo, magonjwa ya kuta za moyo.
Endapo umepata shida na unajua kisababishi ni vema ukaepuka, na kama shida yako hujui kisababishi ni vema kuongea na daktari wako ili upate uchunguzi.
Bonyeza kusoma pia kuhusu makala ya moyo kwenda kasi, kuhisi mapigo ya moyo na kinga na magonjwa ya moyo
Usisahau kuwashirikisha watu uwapendao kupakua app ya ULY CLINIC
Karibu ULY CLINIC kwa tiba na ushauri.
Comments