top of page

Imeandikwa na daktari wa ULY clinic

Dalili za ugonjwa wa seliak

Dalili na viashiria vya ugonjwa wa seliaki ni pamoja na

  • Kuharisha

  • Uchovu

  • Kupoteza uzito

  • Tumbo kujaa gesi na kubeuka

  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Konstipeshen

 

Dalili zingine ambazo zinaweza kuonekana zisizohusiana na mfumo wa chakula ni pamoja na;

  • Upungufu wa damu kutokana na kukosa madini chuma

  • Kupoteza kwa uimara wa mifupa(osteoporosisi)

  • Mifupa kuwa laini(osteomalasia)

  • Kkuwashwa Ngozi

  • Kutokwa na malengelenge na harara kwenye Ngozi (demataitiz hepatifomiz)

  • Vidonda mdomoni

  • Maumivu ya kichwa na uchovu

  • Magonjwa ya mfumo wa neva

  • Maumivu ya maungio ya mwili

  • Kupungua kwa utendaji kazi wa Bandama

 

Dalili zingine zinazoweza kuwapata Watoto ni

  • Kuvimba tumbo

  • Tatizo sugu la kuharisha

  • Kubeuka gesi

  • Kinyesi cha rangi mpauko na kinachonuka kama kimeoza

  • Kutokua vema

  • Kuharibika kwa kichwa cha meno

  • Upungufu wa damu

  • Kuwa msumbufu

  • Kuwa mbilikimo

  • Kuchelewa kubarehe

  • Dalili za mfumo wa neva ikiwa pamoja na ugonjwa wa kutotulia

ULY clini inakukumbusha kwuasiliana na daktari wako wakati wowote kabla ya kuchukua hatua yoyote kulingana na ulichokisoma hapa.

Wasiliana na daktari wa ULY clinik kwa elimu ushauri na tiba kwa kubonyeza hapa ua kupiga namba za simu chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa 12.03.2020

bottom of page