top of page

Virusi

Sehemu hii utajifunza kuhusu Virusi ambao wanaleta magonjwa mbalimbali kwa binadamu

Kirusi chikungunya

Kirusi chikungunya

Kirusi chikungunya ni kirusi anayesababisha homa ya homa ya chikungunya, moja kati ya magonjwa ya mlipuko yanayotokea sana kwenye ukanda wa sana kwenye ukanda wa tropiki kama Afrika na kusini mashariki mwa Asia pamoja na India.

Kirusi herpes simplex

Kirusi herpes Simplex

Kirusi herpes simplex (HSV), ni kirusi kilicho kwenye familia ya Herpesviruses, Familia hii ina virusi wengine ambao ni kirusi varicellazoster, Kirusi cytomegaly, kirusi Epstein–Barr na kirusi human herpes 8- kisababishi cha sakoma ya Kaposi’s.

Kirusi human parainfluenza

Kirusi human parainfluenza

Kirusi human parainfluenza ni kirusi kinachosababisha maambukizi katika mfumo wa upumuaji hasa kwa watoto. Maambukizi hayo ni kama mafua yenye homa, laryngotracheobronchitis , bronkolaitiz na nimonia.

Kirusi zika

Kirusi zika

Kirusi zika ni kirusi anayeenezwa kwa mbu aina ya aedes, mara nyingi huwa hasababishi ugonjwa mkali na dalili zake kuu ni homa, maumivu ya kichwa, misuli, maungio ya mwili na macho mekundu.

Virusi vya UKIMWI

Aina za VVU

Kuna aina mbili za virusi vya UKIMWI, VVU-1 na VVU-2, VVU-1 ambavyo hupatikana karibia duniani kote huwa na kasi ya kusababisha UKIMWI zaidi ya VVU-2 ambavyo hupatikana Afrika Magharibi.

bottom of page